October 8, 2013




Kampuni  inayoongoza  duniani  kwa kutengeneza  vifaa  bora  vya  Elektoniki--Sony,  imeendeleza  dhamira  yake  ya kuleta mageuzi ya kiteknolojia Tanzania, na  safari  hii  imezindua  vifaa  vya  kisasa vyenye  matumizi  rahisi  katika  soko  la bidhaa hizo nchini.


Sony,  inayoongoza  kwa kupendwa na wanamichezo maarufu na watu wengine mbalimbali, pia  katika  soko  la kimataifa  ya  vifaa  vya  Kielektroniki, imezindua  Kamera  tatu  za  kisasa  na televisheni  kubwa  ‘Sony Bravia Full  HD 3D LED TV W8 Series’.


Kamera  zilizozinduliwa  kwa  lengo  la kuleta mageuzi ya kiteknolojia nchini, ni Video  Camera  Sony  Handycam  HDR-PJ380  camcorder,  Kamera  ya  picha za  mnato  Cyber-Shot  HX300  digital still  camera  na  runinga  ya  kisasa  kwa matumizi  ya  nyumbani  (Home  Cinema System- BDV-N9900SH).


Akizungumza wakati  wa  uzinduzi  wa  vifaa hivyo,  mwakilishi  wa  Sony  kwa  nchi za  Mashariki  ya  Kati  na  Afrika,  Rajeev Pallippamadam  alisema  uzinduzi wa  vifaa  hivyo  nchini  Tanzania, unathibitisha  dhamira  ya  Sony kuwekeza  vifaa  vya  kisasa  katika  soka la Kielektroniki.

“Kama  Kampuni,  Tanzania  ni  moja  ya kielelezo  cha  awali  katika  soko  la  vifaa vyetu.  Leo  tunataka  kuwekeza  uzoefu wa  matumizi  ya  vifaa  hivi,  tukitegemea kuwa  watumiaji  watapata  fursa  nzuri na  pana  katika  kutanua  wigo  wa uelewa  wa  vifaa  vya  Sony,”  alisema Pallippamadam.
Uzinduzi  wa  vifaa  hivyo  ni  sehemu  ya mikakati  ya  Sony  kujikita  zaidi  katika kuwekeza  soko  la  vifaa  vyake  barani Afrika,  ambapo  imepanga  kuongeza mtaji  mara  mbili  kufikia  Dola  Bilioni  1.5 mpaka mwaka 2015.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic