November 19, 2013





 Algeria imefanikiwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil baada ya kuichapa Burkina Faso kwa bao 1-0.
 
Kwa ushindi huo, timu hizo zimelingana mabao 3-3, lakini Algeria iliyokuwa nyumbani imepata advantage ya mabao ya ugenini baada ya kufungwa 3-2 katika mechi ya kwanza ikiwa ugenini.

Algeria imekuwa timu ya kwanza ya Afrika Kaskazini kusonga mbele baada ya timu tatu za kwanza, Ghana, Nigeria, Cameroon na Ivory Coast zote kuwa zinatoka Afrika Magharibi.

Bao pekee la mchezo wa leo lilifungwa na Bougherra katika dakika ya 49.

Wageni walicharuka mwishoni, hata hivyo walikosa nafasi zaidi ya mbili ambazo kama wangefunga hata bao moja maana yake wangesonga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic