Mabao matatu yaliyopigwa na Cristiano Ronaldo
yameivusha Ureno kucheza Kombe la Dunia mwakani.
Ushindi huo wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji Sweden
ambao nao mabao yao mawili yalifungwa na nahodha, Zlatan Ibrahimovic.
Katika mechi ya kwanza, Sweden ikiwa ugenini
ilikutana na kipigo cha bao 1-0.
Ureno ilianza kupata bao kupitia Ronaldo,
wenyeji Sweden wakasawazisha na kufunga mabao mawili kupitia Ibrahimovic.
Lakini Ronaldo alipiga mabao mawili harakaharaka
na kumaliza kabisa matumaini ya wenyeji.
0 COMMENTS:
Post a Comment