Mashabiki wa Manchester United wamekasirishwa na
kitendo cha kiungo wa Fulham, Sascha Riether kuonekana akiwa amevaa jezi ya
timu hiyo halafu ametabasamu.
Riether
ndiye aliyemkanyaga kwa makusudi kinda hatari wa Manchester United,
Adnan Januzaj wakati United ilipoitwanga Fulham kwa mabao 3-1, jana.
Alimkanyaga kinda huyo kwa makusudi, lakini
baadaye akaonekana akiwa ni mwenye furaha kubwa na jezi ya Man United ambayo
alibadilishana na mchezaji mmoja wa United baada ya mechi.
Baadhi ya mashabiki wa United waliochangia
kwenye akaunti ya klabu hiyo kwenye mtandao wa Twitter, wameponda wakisema
mchezaji huyo ‘katili’ hakupaswa kuvaa jezi ya timu yao.
Asilimia kubwa ya mashabiki walimuita mnafiki na
muumizaji kwa makusudi, hivyo hakupasswa hata
kupewa jezi ya timu yao.
0 COMMENTS:
Post a Comment