November 7, 2013



Hakuna aliyekuwa akifikiri kwamba mshambuliaji kutoka nchini Burundi atakuwa tishio katika katika Ligi Kuu Bara hasa kwa upachikaji wa mabao.


Lakini sasa Amiss Tambwe wa Simba, raia wa nchi hiyo ndiye anasumbua huku kukiwa na Mrundi mwingine, Didier Kavumbagu wa Yanga pia akionekana kuwa na ubora mzuri.
Mpira una mambo mengi sana, wakati mwingine hisia zinachukua nafasi zaidi kuliko hali halisi, kama kipindi ambacho Yanga walikuwa wakiamini washambuliaji Wakenya ndiyo wanaoweza kuifanya timu hiyo ing’are.

Kumbukia wakati wakiichezea akina Ben Mwalala, Maurice Sunguti au Boniface Ambani. Lakini leo Mganda anaweza kufanya vizuri akiwa katika kikosi hicho.

Hisia za mashabiki au hata walaamu wa soka zinaendana kwa karibu kabisa bila ya kujali ni nchi gani. Ulaya pia mambo hayo yamekuwa yakitokea, wao wanaona ni imani wala si uchawi.
Hivi karibuni kumeibuka mjadala mkubwa kuhusiana na kiungo wa Real Madrid, Gareth Bale kutokea Wales ambayo ni nchi ya asili ya Kingereza.

Kwamba pamoja na kununuliwa kwa gharama kubwa zaidi ya pauni milioni 86 na Real Madrid lakini hawezi kuwa staa zaidi na badala yake atabaki kuwa chini ya Ronaldo.

Wachambuzi wa jarida moja maarufu la michezo wamechambua pia na kusema Bale ataendelea kubaki namba mbili au tatu kwa ubora katika kikosi cha Madrid.

Wachambuzi hao wamerudia nyuma kama ambavyo Watanzania wamekuwa wakiamini mambo tofauti katika michezo, mfano kuamini kutokana na uraia au nchi anayotokea mtu fulani.

Uchambuzi huo unaonyesha hivi, wachezaji wengi kutoka nchi za Kingereza hawajawahi kuwa nyota katika La Liga namba moja katika wakati husika na hasa kama wamesajiliwa na Real Madrid na hiyo inatokana na aina ya uchezaji wao, hata kama watakuwa bora kiasi gani.

Mfano unatolewa wa Steve MacManaman, Michael Owen na David Beckham ambao walitokea England wakiwa nyota wakubwa kwao, lakini Hispania wakashindwa kuwapiku Rau Gonzalez, Figo, Zinedine Zidane na Ronaldo de Lima.

Hali hiyo imeonekana kama ni ushindani wa kitaifa, kwani vyombo vya habari vya nchi za Kingereza zimeonyesha kupingana vikali na namna vyombo vya habari vya Hispania na hata Ureno vinavyochambua.

Baadhi ya wachambuzi wa Uingereza pia wameingia katika hilo na kuonyesha Bale atazima hayo yanayosemwa wakiyaona kama ni zimwi linaloshindika na mwisho mapinduzi yanapatikana.


TAKWIMU
MECHI  MABAO   PASI 

  4                 3            4

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic