November 22, 2013





Uongozi wa Klabu ya Simba umesema kuwa hautalipa faini ya Sh milioni 25 iliyotokana na mashabiki wa timu hiyo kung’oa viti kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar hadi hapo mahakama itakapotoa maamuzi juu ya kesi inayowakabili baadhi ya wanachama wake wanaodaiwa kuhusika.


Simba ilitakiwa kulipa kiasi hicho na serikali kutokana na vurugu zilizotokea uwanjani hapo wakati wa mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar iliyomalizika kwa sare ya 1-1.

Msemaji wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema kuwa wanasubiri mahakama itakavyotoa hukumu juu ya mashitaka yanayoyakabili wanachama wao ambao walitajwa kuhusika katika vurugu hizo.

“Hatuwezi kulizungumzia suala hili kwa kuwa lipo chini ya mahakama, hivyo tutalizungumzia hadi hapo litakapotolewa hukumu kwani kufanya hivyo ni kuingilia uhuru wa mahakama.

“Hatuwezi kulipa kiasi hicho chote kwa sasa kwani kiasi ambacho tunatakiwa kukilipa serikalini ndicho hicho tunachotakiwa kulipa mahakamani, hivyo hatuwezi kulipa fedha zote hizo,” alisema Kamwaga.

Mashabiki 11 wa Simba walikamatwa kufuatia vurugu za uwanjani hapo na kufunguliwa kesi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic