Michuano ya
Uhai Cup inayoshirikisha timu za vikosi vya vijana walio na umri chini ya miaka
20 imeendelea jana na juzi kwenye viwanja mbalimbali huku timu kama za Mbeya
City, Azam FC na Kagera Sugar zikifanya vizuri.
Katika mechi
iliyopigwa jana kwenye Uwanja wa Karume uliopo Ilala jijini Dar, timu ya JKT
Oljoro ilifanikiwa kuichapa Ruvu Shooting kwa bao 1-0.
Aidha, katika
mchezo mwingine uliopigwa juzi kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar timu ya Azam iliifunga
Yanga mabao 2-0, wafungaji wakiwa ni Adam Omari dakika ya saba na Gadiel
Michael dakika ya 39.
Mbeya City
waliichakaza JKT Ruvu ya Pwani kwa bao 1-0, lililotupiwa nyavuni na Gerrard
Mbena dakika ya 80 kwenye Uwanja wa Chuo cha DUCE, Temeke jijini Dar.
Katika
michezo mingine iliyopigwa Karume juzi kwa nyakati tofauti, Rhino Rangers ya
Tabora iliibutua Mtibwa ya Morogoro kwa bao 1-0 huku Kagera Sugar ya mkoani
Kagera ikiikalisha Tanzania Prisons kwa mabao 2-0.
0 COMMENTS:
Post a Comment