November 18, 2013


Uongozi wa Klabu ya Coastal Union, umesema unamtaka kocha mpya wa timu hiyo, Yusuf Chippo, ahakikishe anaipa mafanikio msimu huu.


Coastal imemchukua kocha huyo kwa mkataba wa miaka miwili, baada ya kulitimua benchi lote la ufundi lililokuwa likiongozwa na Kocha Mkuu, Hemed Morocco.

Hatua hiyo imechukuliwa kutokana na kufanya vibaya katika michezo ya Ligi Kuu Bara, wakati viongozi wakiamini wana kikosi cha kutwaa ubingwa.

Katibu Mkuu wa Coastal, Kassim el Siag, alisema wanamtaka kocha huyo ambaye ni raia wa Kenya awape mafanikio ya kumaliza katika nafasi za juu.

Alisema hawana hofu naye kwa kuwa anaijua timu hiyo na alikuwa akihudhuria kwenye mechi zao mbalimbali za ligi kuu walizokuwa wakicheza.


“Ukiangalia tuna pointi chache sana, 16, tupo nafasi ya nane, hivyo tunataka kuona anatupa mafanikio, hiyo itamsaidia na yeye kujiongezea CV (wasifu) yake,” alisema el Siag.     

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic