November 26, 2013




Kura za mashabiki ndizo zitakazomfanya mwakilishi wa Tanzania katika shindano la Project Fame, Elisha Maghiya maarufu kama Hisia aendelea kupeta.
 
Kazi hiyo imeanza leo, kufuatia washiriki wa shindano la Tusker Project Fame kuanza kuchujwa kwa kufuata wingi wa kura kutoka kwa mashabiki, watanzania na mashabiki wa shindano hilo.


Kwa ujumla wanaombwa kumpigia kura Elisha Maghiya (Hisia) mtanzania pekee aliyebaki katika shindano hilo kwa kutuma neno TUSKER 12 kwenda namba 15324 na pia kupiga kura kupitia www.tusker.mob kwani hata akiimba vizuri sana bila kura nyingi zaidi atashindwa kuendelea kuiwakilisha nchi yetu katika shindano hilo.
Kufuatia washiriki kuchuana vilivyo huku kila mmoja akionesha kuwa mkali Zaidi, majaji walijikuta wakishindwa kuchagua ni nani kuingia kikaangoni kwa wiki mbili mfululizo, hivyo kuamua kuwa kwa sasa utaratibu utabadilika na washiriki watatolewa kulingana na idadi ya kura zitakazopigwa na mashabiki wa shindano hilo.

Mshiriki mwenye kura chache atatolewa katika mashindano hayo. Hivyo kufuatia hali hiyo kila mshiriki anategemea mashabiki wake kumuokoa.
Naye meneja wa bia ya Tusker kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti, Saialouise Shayo amewasisitiza Watanzania na mashabiki wa shindano la Tusker Project Fame kumpigia kura mshiriki pekee kutoka Tanzania aliyebaki.

“Hisia ameonesha jitihada kubwa sana katika kuhakikisha anautwaa ushindi wa shindano hilo hivyo tusimuangushe kwani kwa sasa ni kura za watanzania na mashabiki kwa ujumla zitakazomfanya aendelee kufanya vyema katika mashindano ya Tusker Project Fame,” aliongeza Shayo.
Wiki iliyopita Hisia aliimba wimbo wa ‘Big Bad Wolf’ huku akionesha kujiamini na tabasamu zito kama kawaida yake na kuwafanya mashabiki na majaji waridhike na uimbaji wake.
Hisia alitawala jukwaa baada ya Patrick kuimba wimbo wa ‘Nchi Ya Kitu Kidogo’ ulioimbwa na Eric Wainain. Pia alifuatiwa na Nyambura ambae alihitimisha simulizi ya hadidhi yao kwa wimbo wa ‘My Immortal’ ulioimbwa na Evanescence, kwani washiriki hao waliimba nyimbo zao katika staili ya kutoa kisa kinachokamilisha hadithi.      
Jumamosi iliyopita washiriki waliimba nyimbo kutokana na uchaguzi wa majaji. Hii ilitokana na kutokuwepo kwa mshiriki yeyote kikaangoni kwa wiki iliyopita. Hisia alitumbuiza wimbo wa ‘Radioactive’ ulioimbwa na Pentatonix, huku akishirikiana na Amosi na Nyambura wote kutoka Kenya.
Wimbo huo ulikuwa ni chaguo la jaji Ian. Mashabiki na majaji walifurahishwa na uimbaji wa Hisia na kumfanya aendelee kujiwekea nafasi nzuri katika mashindano hayo.
Usikose kufuatilia mashindano haya yanayorushwa kupitia televisheni ya East Afrika TV siku ya jumapili kuanzia saa moja na nusu usiku pamoja na jumamosi kuanzia saa mbili usiku, pia televisheni ya ITV kuanzia saa nne kamili usiku siku ya jumamosi na jumapili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic