November 23, 2013



Na Saleh Ally
Kuna ule msemo kwamba unaweza kuwalaghai watu kwa kipindi fulani, lakini si kila siku.

Binadamu wengi ni welevu lakini wakati mwingine hudanganywa kutokana na uvumilivu au kuamini kwamba mtu fulani anayefanya kitu ambacho si sahihi anaweza kujirekebisha.


Inapofikia wamechoka, basi huwa hakuna ujanja tena na waliosubiri siku zote huwa na msimamo mkali baada ya subira kwisha nguvu.

Mashabiki na wanachama wa Simba wameanza kuonyesha njia kwamba hawafurahishwi na mwenendo wa klabu yao chini ya Mwenyekiti Ismail Aden Rage.

Siku moja tu baada ya kamati ya utendaji ya Simba kumsimamisha mwenyekiti huyo, yeye alijibu mapigo kwamba atarejea.

Watu wengi walijua na kutangaza, kasha wakashadadia kwamba Rage atapokelewa na mamia ya watu kwenye uwanja wa ndege na kisha atakwenda klabuni na kuwapa ‘makavu’ waliomsimamisha.
Lakini mambo yamekuwa tofauti kabisa, angalia idadi ya waliojitokeza kumpokea Rage kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, jijini Dar.

Waangalie wao kwanza, utagundua ni vijana wa aina gani, kwamba wanaonekana wazi walikusanywa kwa ajili ya zoezi hilo.
Hata baada ya kuingia kwenye magari yao matatu waliyokwenda nayo uwanjani pale huku yote yakiwa yamepungukiwa watu, walianza kulalama kuhusiana na posho zao.

Idadi ndogo ya watu hao, ni dalili kwamba Simba wamechoka, wameanza kuamka na wanaona namna gani mwenendo wa timu yao ulivyo.

Wako wanaomtetea Rage, kweli wana haki kwa kuwa pia wanaangalia maslahi yao binafsi.
Lakini wanaotetea maslahi ya klabu yao, kamwe hawawezi kufanya hivyo tena.

Sasa ni dalili tosha ya muonekano wa ukweli kuanza kuchukua nafasi yake, kuwaacha nyuma wale waliokuwa wakiamini kwa kulishwa maneno na sasa watu wataruhusu vichwa vyao vifanye kazi na kutafakari.
Achana na blogu zilizolaghai watu kwamba Rage alipokelewa na mamia ya wanachama, kitu kilichokuwa uongozi mtupu kwa lengo la kutaka kumfurahisha mtu mmoja au kikundi kidogo cha watu wachache au kwa maslahi ya mhusika, yaani mwenye blog.
Ukweli ulionekana, picha zimeonyesha na hata Rage mwenye alijaribu kuuliza kama kweli klabuni palikuwa salama kabla ya kupita.
Hii pia ni nafasi nyingine kuona kwamba mambo yanakwenda tofauti na Simba wengi sasa wameamka na wanataka mabadiliko.

Ukweli usigeuzwe kuwa vibaya, vitisho vikawa msingi badala yake kama mna hoja, hasa mnaomtetea Rage, basi tuendelee kubadilishana hoja na si kutaka kutisha watu na mambo kibao kama risasi, tindikali, huo ni upuuzi mtupu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic