Rais wa TFF, Jamal Malinzi amempa siku
14 mwenyekiti wa Simba aliyesimamishwa kuitisha mkutano mkuu wa dharura wa
wanachama.
Malinzi amemtaka Rage kufanya hivyo mara
moja ili kulipatia usumbufu tatizo la kusimamishwa kwake kwa kuwa TFF imepata
barua kutoka sehemu mbili.
“Tumepokea barua kutoka kwa kamati ya
utendaji ya Simba iliyomsimamisha Rage ikielezea kuhusiana na kusimamishwa
kwake, lakini pia Rage ametupa barua akisema hatambui lolote kuhusiana na hilo.
“Hivyo nimempa ndani ya siku 14 awe
amefanya hivyo ili ufumbuzi wa suala hili upatikane,” alisema Malinzi.
Tayari kamati ya utendaji ya Simba
ilikuwa imeitisha mkutano huo wa wanachama Desemba Mosi ambayo ni ndani ya siku
hizo 14.
0 COMMENTS:
Post a Comment