Kipa Manyika Peter sasa anaendelea
kutesa katika klabu ya Seeb ya Oman.
Manyika ameajiliwa kama mmoja wa makocha
wa makipa katika klabu hiyo nchini Oman.
Akizungumza kutoka Muscat, Oman, Manyika
amesema mazingira ya kazi nchini humo ni mazuri hasa katika suala la vifaa na
utendaji kazi kwa ujumla.
“Huku kuna tofauti kubwa na nyumbani na
hata soka lao lina ushindani mkubwa ukilinganisha na nyumbani.
“Mambo yako vizuri na tunaendelea
kupambana kwa ajili ya mafanikio,” alisema Manyika.
Kipa huyo mkongwe amewahi kudakia Yanga
kwa mafanikio makubwa, pia timu ya taifa Taifa Stars.
0 COMMENTS:
Post a Comment