November 6, 2013


Mashabiki wa Simba wamejitokeza kwa idadi ndogo sana leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Furaha ya ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Ashanti United imeshangiliwa na mashabiki wachache wengi wakiwa na hofu ya kukamatwa na Jeshi la Polisi kutokana na ung’oaji wa viti.


Mashabiki wa Simba waling’oa viti katika mechi waliyotoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Kagera Sugar wakimtuhumu mwamuzi kuwanyonga.
Tayari Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi wa Temeke, linawashikilia mashabiki 11 ambao wanatokea katika vikundi mbalimbali vya ushangiliaji.


Katika mechi ya leo, mashabiki hasa vikundi hivyo walikuwa wachache na ilionekana ni hofu kubwa ya kuingia katika mtego wa polisi kama ilivyokuwa kwa wengine 11 waliokamtwa leo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic