Vijana
wa Simba wanaofundishwa na Kocha Selemani Matola wamewatungua JKT Oljoro katika
michuano ya Uhai Cup inayoendelea kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar.
Mechi
hiyo iliyokuwa kali na ya kuvutia, Simba walitawala zaidi katika kipindi cha
kwanza na kufunga mabao yao yote matatu.
Mabao
ya Simba yalifungwa na Ibrahim Hagib dakika ya 27 na 42 na Miraji Athumani
katika dakika ya 48.
Kipindi
cha pili, kiasi fulani Oljoro walionekana kubadilika lakini bado walishindwa
kuuhimili muziki wa Simba.
0 COMMENTS:
Post a Comment