June 16, 2021


MAKAMU Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Benjamin Kalume, ametaja majina ya wagombea waliopitishwa katika nafasi ya urais ndani ya shirikisho hilo.

Waliopita ni Evans Mgeusa, Hawa Mniga na Wallace Karia, huku Ally Mayay, Ally Saleh na Oscar Oscar wakiondolewa kwenye kinyang’anyiro hicho kwa kushindwa kukidhi kanuni ambazo zilikuwa zimewekwa.

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Agosti 7, mwaka huu jijini Tanga ambapo mbali na nafasi moja ya urais, kuna nafasi sita za wajumbe wa kamati ya utendaji zitagombewa.



Kalume amesema kuwa wanasimamia haki na katiba ya TFF hivyo kwa sasa ni jukumu lao kubandika majina ya wagombea wote ili kujua waliopita kwenye mchujo wa awali.

Aliongeza kuwa ni ruksa kwa wagombea kuleta pingamizi lakini mapingamizi yao yawe na mashiko.

26 COMMENTS:

  1. Sasa kilichobaki ni kumwaga mchanga kwenye ugali maana wao si wamekojolea mboga!!!!!
    LIWWWALLO NA LLIWE!!!!! In Aggrey Mwanry's voice!!!!

    ReplyDelete
  2. Ht iweje hapa,, me naona karia njia nyeupeeeee kuongoza miaka mingine

    ReplyDelete
  3. Mayay imekuwaje wamemwengua, hilo sio sahihi kwa afya ya uchaguzi. Sasa huyo mama ataleta ushindani gani kama sio sawa na uchaguzi wa kisiasa, kupita bila kupingwa

    ReplyDelete
  4. Karia anajitengenezea mazingira. Lakini kiongozi mzuri anatakiwa kushindana na ye yote na kushinda.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mshindani lazima awe na vigezo vilivyowekwa ndo wakina mwakalebela hao kuja kuleta matatizo wakipita

      Delete
  5. Yaani hata huku nako tuumizane vichwa kudai uchaguzi huru na wa haki!!!Dawa ni kupelekana mahakamani tufungiwe na FIFA bila ya kujali ile slogan yao wanayosema eti tuangalie afya ya mpira maana ndio kichaka chao wanachojifichia labda watatambua kuwa watu wamechoka kufanywa wajinga...

    ReplyDelete
  6. Kweli siasa ni nzur ila watu ndio wabaya yaan

    ReplyDelete
  7. Wagombea walioenguliwa ni kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi zilizopo. Haya mambo ya kuanza kulalamika ni ujinga usiomithilika.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Fuatilia vzr uchaguzi usidandie treni kwa mbele, soma kanuni usitake utafuniwe kila kitu

      Delete
  8. Nashauri Mayay aende Mahakamani. Kwanini wamfanyie mizengwe?.

    ReplyDelete
  9. MAYA JAMANI HANA ELIMU, NA KINGINE UYANGA UYANGA NAO SHIDA

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ni nani kakwambia hana elimu? Uchaguzi ukiopita Mayayi alipitishwa na ndiye aliyeleta upinzani mkubwa zaidi. Yaani kipindi kile alikuwa na elimu, leo hana elimu, mmmmh! Au mnataka muendeleze kuendesha soka la Tanzania katika mtindo kama wa kesi za akina Bernard Mirison, eh?

      Delete
    2. Wewe unayejiita SHAIBU inawezekana elimu aliyo nayo Ali Mayai ni zaidi ya kiwango chako cha elimu...

      Delete
    3. Soma kanuni usilete unazili wa kitopolo hapa

      Delete
  10. Ndiyo maana sisi July ligi bado wakati wenzetu tayari Wana ratiba ya msimu ujao ni siasa xa kijinga tu mtu anaamua kujitengenezea maxingira yake karia kapewa kimvuli cha watu ili apite bila kupingwa duhhh


    ReplyDelete
  11. Malipo ni hapa hapa duniani, Haiwezekani uchaguzi mkubwa kama wa tff, Fomu zitoke kwa siku nne tu, na zirudi zikiwa na wazamini,

    ReplyDelete
  12. hapa imetumika kanuni, tar 8 ilitumika "tunasikitishwa"

    ReplyDelete
    Replies
    1. We dada Ngosi acha kumshobokea bwana wako Karia,unajua asipopita na wewe maslahi yako yatakuwa yameenda na kura

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic