MWOMBEKI KATIKA MOJA YA MECHI ZA SIMBA |
Simba imeitwanga Ashanti United kwa
mabao 4-2 katika mechi tamu ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa leo jijini Dar
es Salaam.
Vijana hao wa Msimbazi ndiyo walikuwa wa
kwanza kupata bao katika dakika ya 8 kupitia kwa Ramadhani Singano ‘Messi’
ambaye aliwachambua mabeki, lakini Ashanti wakaonyesha ni wabishi kwa kufunga
bao la kusawazisha katika dakika ya 45 kupitia Hussein Sued.
Timu hizo zilikwenda mapumziko zikiwa
sawa, lakini kipindi cha pili, Simba walionyesha uhai mapema na kupata bao la
pili katika dakika ya pili tu tokea kuanza kwa kipindi hicho, safari hii
Mrundi, Amissi Tambwe akitikisa nyavu tena.
Dakika ya 49 ambayo ilikuwa ni tatu tatu
tu tokea Tambwe afunge, Betram Mwombeki akafunga bao la tatu lakini Ashanti
wakajibu mapigo dakika ya 52, mkongwe Said Maulid ‘SMG’ akionyesha uwezo wake.
Ikionekana kama Ashanti wangeweza
kufanya matokeo hayo kuwa sare, Simba walipata bao la nne na katika dakika ya 89, Ashanti wakapata ‘kimeo’
baada ya kipa wao Amani Simba kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kudaka mpira
nje ya eneo la 18, Daud Mwasongwe akingia kulinda lango baada ya Paul Maono
kutolewa ili aweze kuingia.
0 COMMENTS:
Post a Comment