November 13, 2013


Mashindano ya mchezo wa riadha ya Kilimanjaro yamezinduliwa rasmi leo jijini Dar lakini habari njema ni kuongezwa kwa zawadi kwa washindi.


Meneja wa Kampuni ya Bia ya Kilimanjaro George Kavishe ambao ndiyo wadhamini wakuu amesema katika mbio hizo ambazo pia zitawahusisha watu wenye ulemavu zawadi za safari hii zimeongezeka kwa asilimia 25 ambapo pia kwa Mtanzania yoyote atakayebahatika kuvunja rekodi atazawadia kiasi cha Sh mil 2 zaidi ikiwa kama motisha.


“Tunataka kuona ushindani unaongezeka safari hii ndiyo maana Kilimajaro ikaongeza kiwango cha zawadi tofauti na msimu uliopita, lakini pia hatujawasahu Watanzania nao tumewaka kuhakikisha wanajituma na endsapo yoyote atabahatika kuvunja rekodi atapata kiasi cha Sh milioni mbili zaidi kama motisha,” alisema Kavishe.

Mbio hizo zilizoanzishwa mwaka 2003 zimezinduliwa rasmi mgeni rasmi akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni,Vijana na Michezo Elisante Ole Gabriel katika hafla fupi ilifanyika katika Hoteli ya JB Belmonte.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wawakilishi wa makampuni mbalimbali wa mashindano hayo yatakayofanyika Machi 2 2014 mwakani Ole Gabriel amewasifu waratibu wa mbio hizo kwa kufanya jitihada za kudumisha mbio hizo ambapo zinachangia kukuza sekta ya utalii nchini.

“Takwimu zinaonyesja kwamba takribani raia mbalimbali duniani hushiriki mbio hizi ambao wanatoka Mataifa zaidi ya arobaini duniani, hilo pekee linaleta picha ya kwamba sekta ya utalii inaimarika, niseme kwamba kama kuna lolote mtalihitaji kutoka wizarani msisite kutujulisha.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic