Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania,
Taifa Stars kitawavaa Kenya, Harambee Stars katika mechi itakayochezwa Novemba
19 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Kenya (KFF), Sam
Nyamweya amethibitisha kuwepo kwa mechi hiyo ya kirafiki iliyo katika kalenda
ya Shirikisho la Soka la Kimataida (Fifa).
Akizungumza na SALEHJEMBE jijini hapa,
Nyamweya alisema mechi hiyo ya kujipima nguvu itakuwepo baada ya mashirikisho
hayo mawili kukubaliana.
“Nimezungumza na Rais Malinzi wa TFF,
kila kitu kimekubalika na sasa mechi hiyo itachezwa Dar es Salaam,” alisema
Nyamweya.
Awali kulikuwa na taarifa mechi hiyo
ingechezwa jijini Arusha lakini Kocha Mkuu wa Harambee Stars, Adel Amrouche
akaukataa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa kuwa ni mbaya.
Kweli saa chache baadaye tokea kocha
huyo aukatae uwanja, Bodi ya Ligi Kuu ikatangaza kuufunga kwa madai hauna hadhi
na hasa katika sehemu ya kuchezea.
0 COMMENTS:
Post a Comment