November 27, 2013





Yanga ipo kwenye mazungumzo ya mwisho ya kumsajili mshambuliaji wa kimataifa raia wa Ghana kwa katika usajili wa dirisha dogo.


Dirisha hilo dogo limefunguliwa Novemba 15, mwaka huu ambapo Yanga imepanga kusajili mshambuliaji huyo kabla usajili haujafungwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya kamati ya usajili ya timu hiyo, wanamuongeza mshambuliaji huyo kwa ajili ya kukiimarisha kikosi chao kinachojiandaa na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Chanzo hicho kilisema wakala kutoka nchini huko ndiye anayeshughulikia masuala ya usajili wa mshambuliaji ambaye kabla ya kumsajili watajiridhisha kupitia kwa mitandao ya kijamii ukiwemo wa ‘Youtube’.

“Kamati yetu ya usajili ipo kwenye mazungumzo ya mwisho ya kumsajili mshambuliaji wa kimataifa raia wa Ghana tuliyepanga kumuongeza kwenye usajili wa dirisha dogo.

“Lengo ni kukiimarisha kikosi chetu kinachojiandaa na michuano ya kimataifa, yupo wakala tuliyempa kazi hiyo ya kututafutia mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufunga mabao.

“Licha ya wakala huyo kumpa kazi hiyo, lakini tutajiridhisha zaidi kwa kuangalia video zake za mechi alizocheza akiwa uwanjani kwa njia ya mitandao ukiwemo wa ‘Youtube’, pia ataangaliwa na kocha uwezo wake katika mazoezi yake kabla ya kusaini,” kilisema chanzo hicho.

Alipoulizwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb, alisema wapo kwenye mazungumzo na baadhi ya washambuliaji na wakishakamilisha watawataja hadharani.

“Kiukweli hivi sasa tupo kwenye mazungumzo na baadhi ya washambuliaji tuliopanga kuwasajili kwenye dirisha dogo ambao hatutawataja majina na nchi watakazotoka hadi tutakapokamilisha usajili wao,” alisema Bin Kleb.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic