November 27, 2013





Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) kimetoa masharti kwa wachezaji wa Zanzibar Heroes kufuata sheria na taratibu iwapo watafanikiwa kupata zawadi katika michuano hiyo kwa kutorudia kitendo cha mwaka jana cha kugawana fedha uwanjani.


Heroes walikumbwa na mkasa wa kugawana fedha mwaka jana katika michuano hiyo iliyofanyika nchini Uganda ambapo walifanikiwa kumaliza katika nafasi ya tatu, hali iliyoleta mtafaruku kwa wachezaji kutakiwa kuzirudisha fedha walizogawana ikiwa ni pamoja na kutishiwa kufungiwa kuichezea timu hiyo.

Akizungumza na Championi Jumatano, Rais wa ZFA, Ravia Idarous, alisema kwa upande wao wameiandaa vyema timu hiyo na wanachotarajia ni kuona wanafanikiwa kutwaa kombe ambalo litanogesha sherehe za Mapinduzi na kudai kuwa iwapo watafanya vizuri wachezaji wataruhusiwa kugawana fedha kwa kufuata taratibu.

“Tunachoangalia hivi sasa ni kombe, kuhusu suala la fedha ni mali ya wachezaji ambapo wanatakiwa kufuata utaratibu uliokuwepo katika kugawana.

“Nahodha anachotakiwa kukifanya ni kumkabidhi fedha meneja wa timu kisha wagawane kwani tunachohitaji sisi ni kombe ili liweze kunogesha sherehe za Mapinduzi,” alisema Idarous.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic