Chelsea imeitandika Liverpool kwa mabao
2-1 katika mechi ya Ligi Kuu England iliyopigwa leo jijini London.
Kutokana na ushindi huo, Chelsea
imefikisha pointi 40 na kukwea nafasi ya tatu na kuiporomosha Liverpool hadi
nafasi ya tano ikiwa na pointi 36.
Liverpool ilikuwa ya kwanza kupata bao
kupitia Skrtel lakini Chelsea wakasawazisha kupitia Eden Hazard katika dakika
ya 17 na Samuel Eto’o akamaliza kazi katika dakika ya 34.
Katika kipindi cha pili, Chelsea
ilipoteza nafasi mbili safii ikiwemo ile ya Eto’o ambazo zingeweza kuongeza
wigo wa ushindi.
MATOKEO MENGINE.
Tottenham Hotspurs imeichapa Stoke City kwa mabao 3-0.
Mabao ya Spurs yalifungwa na 'Mzee wa penalti', Soldado, Moussa Dembele na Aaron Lennon.
MATOKEO MENGINE.
Tottenham Hotspurs imeichapa Stoke City kwa mabao 3-0.
Mabao ya Spurs yalifungwa na 'Mzee wa penalti', Soldado, Moussa Dembele na Aaron Lennon.







0 COMMENTS:
Post a Comment