December 30, 2013

KIGGI (WA PILI KULIA) AKIWA NA MWINYI KAZIMOTO, SHOMARI KAPOMBE NA FELIX SUNZU WAKATI WOTE WAKIWA SIMBA. HII ILIKUWA MSIMU ULIOPITA, WOTE HAWA HAWAPO MSIMBAZI KWA SASA.




Kiungo wa Simba SC, Kiggi Makasi, ameonekana akifanya mazoezi  katika Uwanja wa Azam, Chamazi kwa ajili ya kuendelea kuiimarisha zaidi afya yake baada  ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Kiungo huyo alikuwa akisumbuliwa  muda mrefu na tatizo la goti ambalo alikwenda  kutibiwa nchini India na alipewa muda wa miezi mitatu kwa ajili ya uangalizi ili kujua   maendeleo yake kabla ya kurejea uwanjani.
Alipoulizwa Meneja wa Azam, Alando Philipo, sababu ya kiungo huyo wa zamani wa Simba na Yanga kufanya mazoezi na kikosi chao ambapo alidai kuwa alianza muda kidogo kufanya mazoezi katika uwanja huo kwa kuwa anaishi jirani nao hivyo wakamruhusu.

“Kiggi anaishi jirani na hapa na kutokana na hali  yake huwa anakuja hapa kufanya mazoezi tu tena ya peke yake na si ya  kitimu kwa kuwa sio mchezaji wetu bali ni wa Simba,” alisema.
Kiungo huyo alipoulizwa kuhusu hilo alisema: “ Mimi  ni Simba  jamani lakini ninakaa hapo karibu hivyo kutokana na matatizo yangu ndiyo maana nipo hapa nafanya mazoezi  tena peke yangu tu,”alisema Kiggi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic