December 13, 2013


 
MUSOTI AKISAINI JANA MBELE YA KATIBU WA SIMBA, WAKILI EVODIUS MTAWALA
Kipa mpya wa Simba, Ivo Mapunda amesema timu yake hiyo imefanya uamuzi sahihi kumsajili Donald Musoti.
Mapunda amesema beki huyo wa kati ambaye amesaini kuichezea Simba siku moja kama ilivyokuwa kwake ni beki mzuri na wa uhakika.

“Ni wazo zuri, ninaamini Musoti atasaidia kwa kuwa ndiye alikuwa beki wetu tegemeo.
IVO AKISAINI HIYO JANA JIJINI NAIROBI MBELA YA KATIBU MKUU WA SIMBA, WAKILI EVODIUS MTAWALA

“Nafikiri hajacheza mechi chache sana za ligi tokea misimu miwili iliyopita,” alisema Ivo.

Musoti na Ivo walikuwa wanakipiga pamoja na kikosi cha Gor Mahia ya Kenya ambacho walifanikiwa kukipa ubingwa baada ya kuukosa kwa zaidi ya miaka 12.

Wote wawili wametua Simba na tayari wameishaanguka saini.
Wanatarajiwa kuanza kazi Msimbazi mara moja chini ya kocha mpya ‘Mheshimiwa’ Logarusic.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic