December 13, 2013



 
MKINA AKIMILIKI MPIRA, HII WAKATI AKIWA SIMBA (PICHA NA MICHARAZOMITUPU)
Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shija Mkina, amesaini mkataba wa mwaka mmoja wakati huu wa usajili wa dirisha dogo kuichezea JKT Oljoro ya Arusha inayoshiriki Ligi Kuu Bara.


Katibu Mkuu wa Oljoro, Ally Njaidi amesema kuwa lengo ya kumsajili mshambuliaji huyo ni kuiimarisha safu ya ushambuliaji.

“Hadi hivi sasa tumefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shija ambaye tumeingia naye mkataba wa mwaka mmoja, kwa ajili ya kukiimarisha kikosi chetu katika mzunguko wa pili.

“Pamoja na kiungo wa zamani wa African Lyon, Jacob ambaye naye tumeingia mkataba wa mwaka mmoja kama Shija, hivyo tunaamini watakiongezea nguvu kikosi chetu,” alisema Njaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic