December 18, 2013





Kipa mpya wa Simba, Ivo Mapunda na beki, Donald Musoti waliotua Simba wakitokea Gor Mahia ya Kenya, wamesababisha kuibuka kwa vurugu jijini Nairobi.


Beki mpya wa Simba, Donald Musoti, amesema tukio hilo lilitokea Jumamosi ya wiki iliyopita katika Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi wakati Gor Mahia ikiumana na Tusker katika mchezo maalum wa hisani, ambapo Tusker iliibuka na ushindi kwa mikwaju ya penalti 5-3.
Musoti amesema mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo na kuwapungia mashabiki wa Gor, mashabiki hao walichukizwa na uamuzi huo baada ya kuona uzembe wa viongozi wao kwa kuwaachia yeye na kipa Ivo Mapunda.

Anasema mashabiki hao walianza kurusha mawe katika magari ya viongozi wao wakati wakitoka uwanjani hapo, jambo ambalo lilizua taharuki kubwa.
“Ilkuwa hatari sana, unajua kwanza mashabiki hawakuwa wanajua kama tunaondoka kweli, lakini mchezo ulipokwisha, niliwapungia mkono ikiwa ni kuwaaga, hapo ndipo walipoamini kuwa naondoka, walichukia sana,” alisema Musoti.
Taarifa zinasema mashabiki wa Gor hawakufurahishwa na kuondoka kwa wachezaji hao na wanaona kama viongozi wao walikuwa tatizo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic