December 18, 2013





Mshambuliaji mpya wa Yanga, Emmanuel Okwi, kawaida anatumia jezi namba 25 na tayari anayeitumia katika kikosi hicho ametakiwa kuachana nayo.
Okwi aliyekuwa tegemeo Simba, amejiunga Yanga kwa kusaini mkataba wa miaka mwili na nusu na tayari Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) imetua TFF.


Taarifa tulizozipata kutoka ndani ya kikosi hicho, zimesema mabosi wa Yanga tayari wameanza mazungumzo na beki Ibrahim Job, ambaye huvaa jezi namba 25, ili amuachie Okwi anayetarajiwa kutua leo jijini Dar akitokea kwao Uganda.

Mmoja wa viongozi wa timu hiyo amesema Job amekubali kuiachia jezi hiyo kwa masharti kwamba anataka apewe jezi namba 13, hata hivyo imeonekana kuna ugumu kwa kuwa kuna taarifa jezi hiyo tayari imeandaliwa maalum kwa nyota mpya wa kikosi hicho ambaye jina lake halijawekwa wazi.
“Nimepata taarifa viongozi wamemfuata Ibra (Job) wakimtaka aachane na jezi namba 25 ili aweze kupatiwa Okwi, ambaye amekuwa akiitumia jezi hiyo tangu akiwa Simba,” alisema kiongozi huyo.
“Taarifa zilizopo ni kwamba Ibra amekubali, lakini amewataka viongozi kumpatia jezi namba 13, lakini viongozi wanasema atapewa mchezaji mpya ambaye hajajulikana. Hatujajua mwisho utakuwaje,” kilisema chanzo chetu.
Kufuatia taarifa hizo, Championi Jumatano lilimtafuta Job ambaye alikiri kuwepo kwa mpango huo huku akiomba watafutwe viongozi wa klabu hiyo ndiyo watakaoweza kulitolea ufafanuzi zaidi suala hilo.
Okwi aliondoka Simba kwenda kujiunga na Etoile du Sahel baada ya kuuzwa ‘bure’ kwa Sh milioni 480,000, fedha ambazo Simba hawajazipata hadi leo, hali hiyo imesababisha kuamsha machungu kwa wanachama na mashabiki wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic