Kipa Ivo Mapunda na beki Donald Musoti, wote wamesaini rasmi kuichezea Simba
kwa miaka miwili.
Musoti alikuwa pendekezo la kocha Zdravko Logarusic
ambaye pia alinpendekeza Mapunda.
Logarusic ambaye ni kocha wa zamani wa Gor Mahia,
aliwahi kufanya kazi na wachezaji hao wawili akiwa Kenya.
SALEHJEMBE pia iliandika leo mchana na kueleza kwamba Ivo na beki huyo wamekubali kuichezea Simba na usiku wa jana wangemalizana na Simba kupitia kiongozi wake aliyekuwa Nairobi.
SALEHJEMBE pia iliandika leo mchana na kueleza kwamba Ivo na beki huyo wamekubali kuichezea Simba na usiku wa jana wangemalizana na Simba kupitia kiongozi wake aliyekuwa Nairobi.
“Kocha ndiyo amewapendekeza, hivyo hatukuwa na namna
zaidi ya kuwasainisha ili afanye kazi anayotaka,” alisema mmoja wanaohusika na
usajili ndani ya Simba.
Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala ndiye
alisimamia zoezi zima la kuwasainisha Musoti na Mapunda leo hii usiku jijini
Nairobi.
Jana SALEHJEMBE iliandika na kueleza uamuzi wa Simba
kufikia kwenda Kenya.
Na leo ilieleza kwamba tayari kuna ofisa mmoja wa
Simba ameishatua jijini Nairobi kwa ajili ya zoezi hilo.
Ofisa huyo alikuwa ni Mtawala na amelikamilisha na
Ivo aliyekuwa akiitumikia Kili Stars katika michuano ya Chalenji na Musoti
watajiunga na wenzao ndani ya siku mbili kuanza mazoezi chini ya Logarusic.







0 COMMENTS:
Post a Comment