December 18, 2013





Timu ya JKT Oljoro inatarajiwa kwenda kucheza mechi zake za kirafiki jijini Nairobi, Kenya, kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi utakaoanza Januari, 25, mwakani.


Timu hiyo yenye maskani yake jijini Arusha, itaumana na Machava FC ya Moshi inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza kabla ya kutimkia Nairobi mnamo Desemba 24, mwaka huu kwenda kukipiga na timu za ligi kuu ya huko.

Kocha mkuu wa timu hiyo, Hemed Morocco, amesema wanahitaji kucheza na timu za Kenya wakiamini kupata ushindani wanaouhitaji kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili.

"Tutacheza mechi zaidi ya tatu tukiwa Nairobi na timu tofauti, bado hatujajua tutacheza na nani, kuna timu tunaendelea kuzifuatilia kwa ajili ya mechi hizo ambazo tutazitaja muda si mrefu.
"Tumechagua Nairobi kwa kuwa kuna ushindani wa kutujenga kabla ya mzunguko wa pili kuanza, hata hivyo, tutakuja Dar es Salaam pia tukisharudi Kenya kwa ajili ya mechi nyingine za mwisho, tutacheza pia na timu za ligi kuu," alisema Morocco.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic