December 27, 2013




Beki wa kimataifa wa Simba, Joseph Owino amemtaka Mganda mwenzake aliyesajiliwa na Yanga hivi karibuni, Emmanuel Okwi kuachana na vitendo vya starehe ili aweze kuwa katika kiwango kizuri kwa muda wote atakaokuwa na klabu hiyo kwa kuwa hiyo ndiyo siri pekee ya mafanikio yake.


Owino amesema kuwa endapo Okwi hatafanya hivyo, itakuwa ni vigumu kwake kufikia mafanikio aliyoyapata awali wakati akiwa Simba.

Alisema anaifahamu vilivyo tabia ya Okwi kuwa ni mtu wa mambo mengi tangu walipokuwa pamoja SC Villa Uganda na baadaye Simba, ambapo amesisitiza kuwa huu ndiyo muda wa mabadiliko ili afanye kazi na hakuna siri ya ziada ya mafanikio zaidi ya hiyo.

"Kama asipokuwa makini na kuendekeza starehe, mambo yanaweza yakamwendea vibaya na kujikuta asifikie kiwango chake kama alichokuwanacho wakati ule akiwa Villa na baadaye Simba.

"Namjua vizuri sana Okwi, kuwa ni mtu wa mambo mengi lakini anatakiwa kupunguza mambo hayo kwa faida ya soka lake lakini pia asichukiwe na mashabiki wa timu yake mpya ya Yanga," alisema Owino.

Okwi ametua Yanga akitokea SC Villa ya Uganda kwa mkataba wa miaka miwili na nusu na tayari ameanza kuonyesha makali baada ya kuifungia bao timu hiyo katika mechi dhidi ya Simba, Jumamosi iliyopita katika mechi ya Nani Mtani Jembe, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic