Timu ya Majimaji inatarajia kupiga kambi kuanzia kesho Jumamosi katika
mji mdogo wa Peramiho, Ruvuma ili kujiandaa na raundi ya pili katika Ligi
Daraja la Kwanza.
Meneja wa timu hiyo Godfrey Mvula amesema safari hii wamejipanga kucheza
mechi nyingi za kujipima ubavu nje ya mkoa pia amewataka wadau wa soka
kuchangia timu yao kwa moyo mmoja ili kuimarisha timu hiyo ambayo inategemea
bakuli toka kwa wanachama.
Kambi hiyo ipo kwenye eneo la Hospitali ya Peramiho ambapo mara kadhaa
timu hiyo imewahi kuungwa mkono na madaktari wa hospitali hiyo.
“Tunaingia kambini mwisho wa mwezi huu, wadau na wapenda mpira mkoani
Ruvuma wajitokeze kwa wingi kuchangia timu yao kwa kuwa haina fedha na inategemea
toka kwao hivyo lazima wajitoe kwa hali na mali,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment