December 2, 2013


Juhudi za Jeshi la Polisi Kenya kuanza kuwasaka wachezaji wawili wa Eritrea waliozamia zimeanza.

Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye amesema juhudi hizo zimeanza baada ya wapo kuripoti kwa jeshi hilo.

"Tuna matumaini watapatikana na tumeawaachia wao kwa kuwa ndiyo wataalamu, lakini tunaonya hiki si kitu kizuri kwa sifa ya michuano hii," alisema Musonye.
Mapema leo wachezaji wawili wa timu ya taifa ya waliokuwa wanashiriki michuano ya Chalenji nchini Kenya, wametoweka.
Desemba, mwaka jana wachezaji 17 pamoja na dokta wa timu ya Eritrea walitoweka na kuzamia katika mitaa ya jijini la Kampala nchini Uganda.

Lakini mwaka 2009, hali ilikuwa hivyo hivyo baada ya wachezaji wengine kuzamia nchini katika jiji la Dar es Salaam.

 Musonye alithibitisha kutoweka kwa wachezaji hao wawili wa Eritrea.

“Walishindwa kurejea hotelini tokea jana na wenzao wamesema watakuwa wamepotelea katika mitaa ya Kenya,” alisema Musonye.

Imeelezwa maisha katika nchi ya Eritrea yamekuwa si mazuri na ubabe wa serikali umekuwa chanzo cha vijana wengi kuamua kutorejea kwao.

Mwaka jana Kitengo cha Haki za Binadamu cha Umoja wa Mataifa kupitia Mkuu wake, Navi Pillay kiliilaumu serikali ya Eritrea kutokana na uonevu na unyanyasaji.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic