December 14, 2013





Kipa bora namba moja nchini Juma Kaseja, leo aliporomosha dua wakati mwamuzi akijiandaa kuanzisha mechi ya kirafiki kati ya Yanga iliyokuwa inawavaa KMKM ya Zanzibar.


Katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Kaseja alikuwa anacheza mechi yake ya kwanza tokea arejee Yanga.

Wakati mwamuzi akijiandaa kuanzisha mchezo, Kaseja aliinua mikono na kuanza kusali na alifanya hivyo kwa takribani dakika moja, hadi pale mwamuzi alipopuliza filimbi kuanza mechi, ndiyo akahitimisha sala yake.
Mechi ilimalizika kwa Yanga kushinda kwa mabao 3-2, Kaseja akiwa ameanza dakika 90 za kwanza Yanga kwa kufungwa mabao mawili.
Hata hivyo, Kocha Ernie Brandts alimsifia kwa kuonyesha kiwango kizuri huku akisema uzembe wa mabeki ulisababisha Yanga kuruhusu mabao hayo mawili.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic