December 23, 2013


Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog, ameomba mechi tano za kirafiki kabla ya michuano ya Kombe la Mapinduzi kuanza mnamo Januari 2, mwakani.


Kocha huyo aliyesaini kuifundisha Azam hivi karibuni akichukua nafasi ya Muingereza, Stewart Hall, anataka mechi hizo kwa lengo la kuona viwango vya wachezaji wake na kuteua kikosi cha kwanza.

Katibu Mkuu wa Azam FC, Idrissa Nassoro, alisema kocha wao ameomba mechi tano za kirafiki na wana imani kuwa zitaisaidia Azam kutetea Kombe la Mapinduzi.

“Kocha Omog ametaka mechi tano za kirafiki kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Mapinduzi ili kukitayarisha kikosi chake na kufanikiwa kutetea kombe letu.

“Kocha amekuja na falsafa mpya ambapo anahitaji kukibadilisha kikosi ili kiweze kuwa imara hadi kwenye ligi kwa kuhakikisha tunamaliza katika nafasi nzuri.

“Lengo letu ni kuona tunafanikiwa kutetea Kombe la Mapinduzi, ndiyo maana tunajiandaa vya kutosha kuhakikisha tunafanikisha lengo letu,” alisema Nassoro.

Kocha huyo alitarajiwa kutua Ijumaa iliyopita kwa ajili ya kuanza rasmi kazi ya kukinoa kikosi cha Azam ambacho kwenye Ligi Kuu Bara kipo katika nafasi ya pili kikiwa na pointi 27.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic