Kiungo mshambuliaji wa Simba, Uhuru
Selemani, juzi alijikuta akimpiga ngumi shabiki wa Yanga, baada ya kuambiwa
maneno machafu katika mchezo baina ya timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Tukio hilo lilitokea nje ya uwanja
ambapo Uhuru alikuwa akienda kumsalimia mshambuliaji wa Yanga, Emmanel Okwi
aliyekuwa na shabiki huyo, ndipo alipokutana na lugha chafu.
Shabiki huyo aliyekuwa kavua jezi huku
mgongoni kajiandika ‘Ngassa+Okwi Sawasawa na Kifo’, hakufurahishwa na kitendo
cha Uhuru kusalimiana na Okwi ambaye alikuwa akiongea naye, ndipo akamwambia:
‘Nyie Simba wachawi’, kitendo kilichomuudhi nyota huyo wa Simba aliyekuwa
amembeba mtoto wake ambapo alimuweka chini na kumrushia ngumi kali.
Baada ya timbwili hilo kutokea, Okwi
alimuomba Uhuru atulie, aachane na shabiki huyo ndipo Uhuru aliaga na kuondoka
kwa hasira eneo hilo.
0 COMMENTS:
Post a Comment