December 14, 2013



Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema ikiwezekana ataingia mapema na kuisubiri Yanga.

Logarusic amesema anataka kuiona Yanga ikicheza angalau mechi moja kabla ya mechi yao ya Nani Mtani Jembe, Desemba 21.
 
“Nataka nione mwendo wao ukoje, nikiweza nitafika mapema zaidi kwa kuwa nataka nione mechi yote au kipindi kimoja.
“Lakini sehemu muhimu ninayotaka kuona ni namna watakavyocheza mwanzo, kuna mambo muhimu ya kuangalia,” alisema.
Kocha huyo aliamua kubadili program yake ya mazoezi ili leo aende akaione Yanga ambayo itakuwa mechi yake kubwa ya kwanza atakapokutana nayo Desemba 21.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic