December 14, 2013





Mshambuliaji nyota wa zamani wa Man United, Andy Cole amesema program na promosheni zinazoandaliwa na kampuni ya simu ya Airtel zinaweza kusaidia mabadiliko makubwa katika soka nchini.


Cole amesema hayo leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar.

Kufikia mafanikio si kitu lahisi, kwanza lazima kuwe na watu wenye ndoto na wanaotaka kuzifuata.



Kabla ya kufikia ndoto zako lazima ujitume kwanza. Nimeona Tanzania kuja vipaji vingi sana tokea nilipokija mwaka 2011 kwa ajili ya Airtel Rising Star.

Hizi program za Airtel ni sehemu ya changamoto kusaidia kwenda juu, inawezekana kabisa Tanzania ikawa na mchezaji Premiership na akafanikiwa, alisema.

Mkali huyo wa mabao England, kesho atakuwa Karume kugawa mipira kwa watoto na baada ya hapo, atasepa hadi Coco Beach ambako ataangalia mechi pamoja na wadau.
Mechi atakayoangalia ni kati ya Man U dhidi ya Aston Villa.








0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic