December 28, 2013




Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic ameendelea kulia kwamba hapendi kuzungumia wachezaji wa timu nyingine.
 
Akizungumza na SALEHJEMBE kutoka Croatia, Logarusic amesisitiza kwamba hana mpango hata kidogo kutaka kuzungumzia wachezaji wa timu nyingine kama ilivyoripotiwa na gazeti la Mwanaspoti.
“Nimesoma na nimezungumza na baadhi ya rafiki zangu, kwamba mimi siwezi kuzungumzia wachezaji wa timu nyingine.
“Hakikuwa ni kitu kizuri kabisa, kunisingizia maneno yale. Nimesomewa kwamba ningepewa Yanga basi ningewafukuza mabeki wote, si kweli.
“Nimekasirika sana, nilitamani nirudi Tanzania kufafanua suala hilo,” alisema.
Baada ya gazeti hilo kuandika, siku iliyofuata taarifa zilizagaa kwenye mitandao zikieleza kukasirishwa kwa kocha huyo.
Logarusic alimtumia ujumbe msemaji wa zamani wa Simba, Ezekiel Kamwaga alilalama kuhusiana na habari hiyo.
Kamwaga akaitundika kwenye ukurasa wake wa Facebook ingawa mara baada ya watu kuanza kuandika wakiliponda gazeti hilo la michezo, akaitoa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic