Kazi
anayotakiwa kufanya kocha wa timu imeonekana wakati wa mechi ya watani, Simba
na Yanga walipovaana katika kipute cha Nani Mtani Jembe.
Kocha Mkuu
wa Simba, Zradvko Logarusic, alionyesha ni anayejiamini, anayeweza kufanya
uamuzi mara moja bila ya kuchelewa na kweli timu yake ikashinda.
Katika
mechi ya juzi kwa kuwa ilikuwa ni kama ya kirafiki, kila timu ilipewa nafasi ya
kubadili wachezaji sita, Logarusic akawaonyesha wachezaji wa Simba kwamba
katika kikosi chake, hakuna staa zaidi yake.
Kocha huyo
raia wa Croatia alifanya mabadiliko yote sita, lakini burudani kubwa ilikuwa ni
namna alivyowabadilisha wachezaji hao bila ya kupoteza muda hata kidogo, hata
kama kosa lingeonekana ni dogo kwa mashabiki.
Kweli
hataki mchezo kwa kuwa mabadiliko yake ya kwanza yalianza katika dakika ya 26
alipomtoa Said Ndemla ambaye alichezeshwa namba 10 iliyoonyesha kumshinda,
nafasi yake mara moja ikachukuliwa na Ramadhani Singano ‘Messi’ ambaye
aling’ara vilivyo.
Dakika tano
baadaye, Logarusic akamuita mkongwe Henry Joseph kwenye benchi, kisa? Alikosea
pasi moja tu ambayo ilionyesha hayuko makini, akapumzishwa na nafasi yake
akachukua Ramadhani Chombo ‘Redondo’.
Hiyo ni
rekodi mpya kwa kocha kufanya mabadiliko ya wachezaji wawili katika mechi ya
watani Yanga na Simba na huenda kama angepoteza mchezo basi angekuwa kwenye
lawama kubwa. Yeye mwenyewe anasema hajali presha badala yake ni kazi.
“Nilijua
lolote linaweza kutokea lakini huo ni ujumbe kwa wachezaji wangu kwamba nataka
wafuate maelekezo yangu bila ya visingizio,” anasema Logarusic.
Kweli
alionyesha hajali kwani kipindi cha pili alifanya mabadiliko mengine manne,
akianza na dakika ya 56, yaani dakika 11 tu baada ya kuanza kipindi cha pili,
akamtoa Haruna Chanongo baada ya kutoa pasi kizembe, akaingia Uhuru Selemani.
Dakika
mbili baadaye akampumzisha Amissi Tambwe ambaye alikuwa amefunga mabao mawili
ambapo Simba ilikuwa inaongoza wakati huo, nafasi yake ikachukuliwa na Amri
Kiemba.
Dakika ya
73, akamtoa Awadhi Juma aliyekuwa ameumia na kumuingiza Zahoro Pazi na baadaye
dakika ya 84 akamtoa Chombo aliyeingia kuchukua nafasi ya Henry na kumuingiza
Abdulhalim Humud kuongeza ulinzi ili kulinda mabao.
Inawezekana
mabadiliko hayo yalitokana na kocha huyo kuwa na nafasi ya kubadilisha watu sita,
lakini hata ingekuwa watatu tu, bado ni sehemu ya kuonyesha kocha anapaswa
kujiamini kiasi gani, kuwa na uamuzi wa haraka na kujiamini.
“Mimi ndiyo
kocha, naona kipi sahihi katika wakati upi. Naweza kufanya mabadiliko na kitu
kisiwe kizuri, lakini bado natakiwa kufanya kazi si kwa kuangalia hisia za
mashabiki au viongozi na kila mmoja ajue kila ninachoamua ni kwa ajili ya kitu
kizuri cha timu, si mimi binafsi,” anasema Logarusic akionyesha kujiamini.
Siku mbili
kabla ya mechi, Logarusic aliwaondoa wachezaji wengine kwenye kambi wakiwemo
nyota kama Gilbert Kaze na Betram Mwombeki. Wengi waliona ajabu lakini mwisho
ametimiza alichotaka na kujenga kuaminiwa.
Championi
lilikuwa la kwanza kukataa kocha mpya wa Simba hakuwa yule aliyetangazwa
mwanzo, lakini likamuelezea Logarusic na misimamo yake, sifa yake kwa mashabiki
wa Gor Mahia ya Kenya, namna wanavyomthamini na kufikia kusema ubingwa wao
walioupata chini ya kocha Bobby Williamson, Logarusic ndiye anastahili kwa kuwa
alijenga timu.
Sifa zake
ni ujeuri lakini ameonyesha ni wenye manufaa na makocha wanatakiwa kuwa wenye
uwezo wa kuamua na wakikosea wakubali makosa.
atufikishe pale tunapopataka tutampenda zaidi
ReplyDelete