PAZI (KUSHOTO) AKIBAKI AMESHANGAA BAADA YA KASEJA KUMPA JEZI YAKE, HALAFU YEYE HAKUTAKA KUCHUKUA YAKE NA BADALA YAKE AKASALIMIANA NA KIEMBA NA CHOMBO NA KUONDOKA ZAKE. |
Huku
ikionekana ni hofu baada ya kufanya kosa lililozaa bao la tatu la Simba, kipa
wa Yanga, Juma Kaseja, alikataa kuipokea jezi ya Zahoro Pazi wa Simba mara
baada ya mechi ya Nani Mtani Jembe.
Katika mechi
hiyo iliyochezwa Jumamosi na Yanga kulala kwa mabao 3-1. Kaseja alikataa
kuchukua jezi ya Simba.
HAPA WAKATI AKIVUA JEZI NA KUMPA PAZI.. |
Huenda
alihofia kuonekana ameishika na mara baada ya kubadilishana na Zahoro Pazi,
yeye alimpa yake lakini akakataa kuchukua ya Simba na kuondoka zake.
Daktari
mkongwe, Shecky Mgazija alionekana kumpoza kwamba alichofanya ni kosa la
kimichezo lakini Kaseja alionekana kama ni mtu aliyechanganyikiwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment