December 2, 2013


Mabao mawili ya Emmanuel Okwi na moja la Hamis Kiiza yametosha kuwaondoa mashindanoni Ertirea.

Uganda, The Cranes imeibabua Eritrea kwa mabao 3-0 katika mechi ya michuano ya Chalenji iliyopigwa jijini Nairobi, Kenya.

Okwi ndiye alikuwa wa kwanza kuifungia bao kupitia pasi ya Sserunkuma, Kiiza akafunga la pili kwa mkwaju wa penalti baada ya Sserunkuma kuagushwa.


Sserunkuma alitoa pasi nyingine kwa Okwi ambaye alimalizia kazi na kuwafanya vijana wa Micho wafuzu kwenye hatua ya robo fainali wakitokea kundi C.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic