Rwanda
imefungwa mechi ya pili mfululizo katika michuano ya Kombe la Chalenji, maana
yake haina nafasi ya kusonga mbele.
Michuano hiyo inaendelea nchini Kenya na timu za Zanzibar na Bara ni kati ya zinazoshiriki na kila moja imeonja ushindi.
Leo Rwanda
maarufu kama Amavubi imefungwa kwa bao 1-0 na Sudan ikiwa ni mara ya pili baada
ya kupoteza kwa idadi hiyo dhidi ya Uganda.
Juhudi za
nahodha, Haruna Niyonzima aliyeonekana kuhaha uwanja mzima baada ya Salah
kuifungia Sudan bao, hazikuzaa matunda.
Mechi
ilikuwa nzuri lakini Sudan walionekana kujipanga vizuri kiufundi na kuizuia
Amavubi kwa dakika zote 90.
0 COMMENTS:
Post a Comment