Kikosi cha Kilimanjaro Stars kimepata
ofa kubwa baada ya kupewa zawadi nono ya mamilioni na Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF).
Zawadi hiyo imetolewa na Rais wa TFF,
Jamal Malinzi amsema tayari alishazungumza na nyota wa timu hiyo kupambana na
endapo watafanikiwa kuchukua ubingwa, kikosi hicho kitagawana zawadi ya bingwa,
kiasi cha dola 30,000, sawa na Sh milioni 48.
Malinzi amesema ofa hiyo haitaishia hapo.
Wakishika nafasi ya pili watagawana dola 20,000, sawa na Sh milioni 32 na wakiambulia
nafasi ya tatu watapata dola 10,000 (Sh milioni 16).
“Nawapongeza sana Stars kwa ushindi huo
lakini wanatakiwa kujua kwamba safari bado ndefu, Watanzania wanataka ushindi
kwa kuchukua ubingwa, hivyo wanatakiwa kupambana na kuhakikisha wanalileta taji
hapa nchini,” alisema Malinzi.
“Nilishawaeleza mapema katika mkutano
wangu na timu hiyo tukiwa kule Nairobi wakati nikihudhuria mkutano wa Cecafa
kwamba kama wakifanikiwa kushika nafasi tatu za juu kuanzia bingwa, mshindi wa
pili na ile ya watatu, watachukua fedha zote na kugawana wao, mimi sitaki
kuziona hizo fedha TFF, ni za kwao, kazi kwao kupambana sasa.”
Tayari kikosi hicho kimeshatinga hatua
ya nusu fainali ya michuano hiyo ya Kombe la Chalenji inayoendelea jijini
Nairobi nchini Kenya ambapo kesho kitavaana na Kenya.
SOURCE: CHAMPIONI







0 COMMENTS:
Post a Comment