December 14, 2013




Timu ya Seeb Club ya Oman imeendelea kutesa katika ligi kuu ya nchi hiyo.
Seeb anayoifundisha Mtanzania, Manyika Peter imefanikiwa kuwachapa vigogo Fanja kwa bao 1-0.

Manyika ambaye ni kocha wa makipa wa timu hiyo amesema baada ya kushinda mchezo huo mwishoni mwa wiki, sasa wanafunga safari kwenda mkoa mwingine.


“Tunasafiri kwenye mkoa mwingine kuendelea na ligi ingawa kutakuwa na ushindani mkubwa, unajua mnaposhinda dhidi ya timu kongwe kama hizo basi lazima timu mnayocheza nayo inapania sana.

“Lakini tuna kikosi kizuri na tumejiandaa vilivyo kwa ajili ya kucheza vizuri na kushinda,” alisema Manyika kutoka nchini Oman.


Wakati akiwa mchezaji, Manyika aling'ara akiwa na Yanga, Mtibwa Sugar, Kili Stars na Taifa Stars.
 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic