December 14, 2013

AMROUCHE, ALIYEBEBA KOMBE AKIWA NA MSAIDIZI WAKE



Kocha Mkuu ya Kenya, Adel Amrouche amesema ametwaa Kombe la Michuano ya Chalenji, si kwa bahati.
 
Amrouche raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria amesema pamoja na kutokuwa na maandalizi ya kutosha sana, lakini kujituma kwa wachezaji na benchi la ufundi, kumezaa matunda.

“Tulitaka kulitwaa kombe hili, kila mmoja alijituma na tulifanya kazi kwa kutaka kutimiza malengo.
“Tulijua Wakenya wote walisubiri mafanikio yetu nasi tukapambana vilivyo,” alisema Amrouche.
“Tuliweza kuzifunga timu zote bora ikiwemo Tanzania na Sudan, mwisho sisi ndiyo tumekuwa bora kuliko wengine.
“Nawashukuru wachezaji wangu, watu wa benchi la ufundi na wote waliojituma kwa ajili ya mafanikio kwa Harambee Stars,” alisema Amrouche aliyeonekana kuwa kocha bora zaidi katika michuano hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic