December 16, 2013



BAHANUZI (KULIA) AKICHUANA NA JAVU


Mshambuliaji wa Yanga Said Bahanuzi bado anahitajika nchini Malsyia baada ya klabu nyingine kuonyesha nia ya kuhitaji huduma yake.

Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto, amesema Bahanuzi alikuwa nchini humo siku tano zilizopita, akipelekwa  kwa lengo la majaribio katika klabu ya Terrenganu FA, inayoshiriki ligi kuu nchini, lakini klabu nyingine ya T Team imejitokeza katika nia ya kumuwania mshambuliaqji huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar.
Kizuguto, amesema awali T Team ilimuona Bahanuzi wakati ikicheza mchezo wa kirafiki na Terrengan, lakini ilitaka mshambuliaji huyo kurudi nchini kwanza kabla ya kupewa mualiko mpya, utakamrudisha Malsyia kumalizia hatua ya mwisho kabla ya kusajiliwa.
“Ikumbukwe kuwa, Bahanuzi alishafanya mjaraibio na Terrenganu lakini wakati akiwa huko, klabu hiyo ilicheza mchezo wa kirafiki na hiyo T Team, ambao nao waliopoonyesha kumuhitaji mchezaji wetu, katika hilo wakaona kwanza amalize majaribio ya sasa na akirudi huku watamtua mualiko mwingine kurudi huko,” alisema Kizuguto.
“Kwasasa Bahanuzi tunaye hapa kutokana ni mchezaji ambaye yupo kwenye mipango yetu na kama T Team wakituma huo mualiko tutampa ruhusa ya kurudi huko haraka kutafuta bahati yake ya kucheza soka la kulipwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic