December 8, 2013


 
MAJUKWAA
Kwa muda wa miezi kadhaa SALEHJEMBE imekuwa ikitoa makala mbalimbali zikielezea na kuonyesha mazingira ya viwanja vinavyotumika katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara. 


Wakati fulani ilifikia hadi Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) kutangaza kuvifungia baadhi ya viwanja hivyo. TFF imeeleza sababu mbalimbali na kuwataka wahusika wafanye marekebisho yanayotakiwa, la sivyo timu zinazotumia viwanja vilivyofungiwa zitalazimika kutovitumia.
 
GETI KUBWA LA MAGARI
Lakini inawezekana TBL ilipitiwa na kuusahau Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi ulisahaulika, maana hauna hadhi ya kuchezewa Ligi Kuu Bara.
Swali, TPL walihofia kwa kuwa unatumiwa na timu za jeshi, au walipitiwa tu?

Uwanja wa Mabatini uliopo Mlandizi Pwani nao unatumiwa katika baadhi ya mechi kwenye ligi hiyo, ukiwa ni uwanja wa nyumbani wa Ruvu Shootings, lakini haumo kwenye orodha ya vile vilivyofungiwa.
 
BENCHI LA RUVU SHOOTING

BENCHI LA KAGERA

Uwanja huo upo umbali wa kilometa moja kutoka kituo cha daladala cha Mlandizi. Maji ya kumwagilia yapo na hiyo imesababisha sehemu ya kuchezea kuwa na ubora mzuri kwa kuwa nyasi ni nyingi na zinavutia.
 
KAGERA WAKIINGIA UWANJANI
Pamoja na uzuri huo wa sehemu ya kuchezea, sehemu ya majukwaa haina ubora mzuri na kuna sehemu ambazo zinaonyesha wazi hazijafanyiwa ukarabati kwa muda mrefu.

Kuna jukwaa ambalo limegeuzwa kuwa sehemu ya kujisaidia, wakati wa mechi kuna wachezaji na mashabiki ambao wamekuwa wakisimama hapo kisha kujisaidia haja zao na wengine kuoga kabisa.
 
GETI LA MASHABIKI KUINGILIA UWANJANI
Uzio uliozunguka uwanjani hapo nao pia ni kama wa kuunga-unga, matundu ni mengi na endapo kunatokea purukushani basi madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Siku ya mechi ya Ruvu Shooting dhidi ya Kagera Sugar, mwezi uliopita, kuna tiketi zilizoonyesha kuwa zinatakiwa kuuzwa kwa Sh 3,000 lakini ziliuzwa kwa Sh 2,000, gazeti hili lilipouliza wahusika hakuna aliyekuwa na jibu.

Kuna mashabiki wachache waliokuwa wamekaa nyuma ya lango la upande wa magharibi waliokuwa wakivuta ‘sigara kubwa’ na hakukuwa na hatua zozote walizochukuliwa wala kuzuiliwa.

Lango kuu la kuingilia uwanjani hapo ni la bati na halina ubora mzuri. Kwa hali halisi kuna sababu nyingi za TFF kushirikiana na wamiliki wa viwanja kuendelea kuboresha viwanja ili viendane na hadhi ya ligi husika.

Angalia vizuri picha na uone hali ilivyo mbaya katika uwanja huo, hakika si hali nzuri na imepitiliza. TPL, hebu fanyeni ziara au tumieni picha hizo kuona maana inawezekana mlipitiwa tu!

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic