January 5, 2014





Kipa Yaw Berko raia wa Ghana, amemuambia Kocha wake, Zdravko Logarusic kwamba akimpa nafasi naye ataonyesha uwezo.
Kocha huyo raia wa Serbia alisema jana ataanza kumpa nafasi Berko katika mechi ya leo ya michuano ya Mapinduzi dhidi ya KMKM.
 
“Kama nitapata nafasi litakuwa jambo zuri, nitaifanyia kazi na kocha akiwa kwenye benchi naamini atafurahi,” alisema Berko.
Logarusic amekuwa akimtumia kipa Ivo Mapunda ambaye aliwahi kufanya naye kazi kwenye kikosi cha Gor Mahia ya Kenya.

Berko ameingia mkataba wa miezi sita kuidakia Simba na baada ya msimu huu atalazimika kuondoka kwa kuwa TFF imepitisha sheria ya wachezaji watatu wa kimataifa lakini hakuna golikipa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic