January 5, 2014



 
SINGANO AKIWA NA LUHENDE
Winga mwenye kasi wa Simba, Ramadhani Singano ‘Messi’ amesema hawezi kuvimba kichwa kutokana na mafanikio anayoyapata.

Akizungumza na SALEHJEMBE, Messi alisema yeye ni mtu anayejali mafanikio lakini anathamini mchango wa watu.
“Ninaishi na watu na ndiyo wanaonisaidia kuendelea, hivyo siwezi kuwa na dharau.
“Lakini kitu kizuri lazima nao waamini mimi ni mwanadamu, ikitokea nimekosea basi wanielewe,” alisema.

Messi amekuwa gumzo kutokana na uwezo ambao amekuwa akiuonyesha katika mechi mbalimbali.
Katika michuano ya Mapinduzi inayoendelea mjini Zanzibar, Messi amekuwa kati ya wachezaji gumzo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic