January 9, 2014

BOBAN (WA TATU KUSHOTO) AKIWA NA WACHEZAJI WENZAKE WA COASTAL UNION KWENYE MSTARI WA KUINGIA NDANI YA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA JULIUS NYERERE.

Kiungo wa Wagosi wa Kaya, Coastal Union, Haruna Moshi ‘Boban’ ameondoka leo na kikosi hicho kwenda kwenda Oman kuweka kambi kujiandaa na Ligi Kuu Bara.


Boban alikuwa katika muonekano tofauti kabisa na ilivyokuwa awali baada ya kunyoa rasta zake.

Kawaida Boban amekuwa akionekana na rasta hizo, lakini leo ilikuwa tofauti kabisa.

Hali hiyo ilisababisha mashabiki waliokuwa uwajani hapo kushindwa kumtambua huku wengine wakidhani hakuwa kwenye msafara huo.


Coastal Union wameondoka leo mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar wakiwa na kikosi chao kamili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic