January 31, 2014


Kiungo Athumani Iddi ‘Chuji’ amerejeshwa kundini na kufanikiwa kujiunga na wenzake wanaojiandaa na mechi dhidi ya Mbeya City.


Chuji amejiunga na Yanga ambayo imeweka kambi mjini Bagamoyo baada ya mchezo wake dhidi ya Coastal Union mjini Tanga uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mkongwe huyo katika kugawa mipira, aliomba radhi kwa viongozi, benchi la ufundi na wachezaji wenzake kwamba kitendo alichokifanya hakikuwa sahihi.

Chuji alisimamishwa kwa mda usiojulikana kutoana na utovu wa nidhamu na SALEHJEMBE ilikuwa ya kwanza kuanika kwamba kusimamishwa kwake kulitokana naye kuondoka wakati kikosi kikiwa uwanjani kinapambana katika mechi ya Nani Mtani Jembe.
Kiungo huyo mwenye uwezo wa kupiga pasi za mbali zinazofika kuliko mwingine yoyote nchini, atakuwa amekutana kwa mara ya kwanza leo na Kocha Mkuu, Hans van Der Pluijm ambaye amejiunga na Yanga wakati yeye akiwa kifungoni.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic